Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Viwanda na Biashara
Mwisho: 14th Sep 2020
Request for Consultancy To Review and Develop National Policy and Legal Framewor...
Mwisho: 28th Apr 2020
Request for Expression of Interest Title: Consultancy to Develop a National Dat...
Imewekwa: 15th November, 2020
Wanafunzi wa Tanzania wanaosomea Jiangxi, wameshiriki Maonesho ya Kitamaduni ya Kimataifa ya International Cultural Festival (ICF) yaliyofanyika tarehe tarehe 14 Novemba, 2020 nchini China. Maonesho hayo ambayo hufanyika mara moja kwa mwaka yalifadhiliwa na Chuo Kikuu cha Jiangxi cha masuala ya Fedha na Uchumi (JUFE) ambapo yaliwakutanisha wanafunzi wanaoziwakilisha nchi zao, wafanyabiashara na raia mbalimbali wa nchini China. Katika maonesho hayo wanafunzi wa Tanzania waliweza kuonesha fursa za uwekezaji na biashara katika bidhaa za Korosho, Utalii, mapishi ya chakula cha asili cha Tanzania na madini ya Tanzanite ambapo banda la Tanzania lilikuwa ni miongoni mwa vivutio kutokana na maandalizi yake ambapo lilihusisha utalii wa Tanzania kwa kuonesha picha za video na vipeperushi vilivyotolewa na ubalozi wa Tanzania nchini China. Katika maonesho hayo kundi la wanafunzi wanaosomea Uzamili kutoka Tanzania ambao pia ni watumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiongozwa na afisa biashara kutoka wizara ya Viwanda na Biashara ndugu, David Geofrey walishiriki kuandaa banda la Tanzania.